Friday, February 7, 2014


Stori: Gladness Mallya
BAADA ya mwanamuziki Baby Joseph Madaha kunaswa na mtego wa kujiuza uliotegwa na gazeti hili hivi karibuni, mdada huyo anaonekana kubadilika na anadai mgogoro uliojitokeza kati yake na meneja wake, Joe Kairuki kutokana na tukio hilo umekwisha.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni msanii huyo ambaye ni kati ya wasanii wa kike wanaofanya vizuri alisema, tukio lile limefanya ajifunze kitu na kubadilika kwake kumesababisha bosi wake amsamehe na waendelee kupiga mzigo.
“Kweli nimejifunza kutokana na makosa maana kunaswa kwenye ule mtego kumenigharimu sana lakini nashukuru nimesamehewa na mkataba ninaendelea nao, yale yamepita na sasa ni kazi tu,” alisema Baby Madaha a.k.a The Queen of Swaga.

0 comments:

Post a Comment