Monday, February 10, 2014


Stori: Na Igenga Mtatiro, Tarime
MDUNGUAJI wa watu takriban tisa wilaya ya Tarime mkoa wa mara, alifariki dunia usiku wa kuamkia juzi alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime baada ya kuzidiwa na vipigo vya Jeshi la Polisi, akigoma kutaja washirika wake.
Taarifa zilizotolewa na mganga mfawidhi wa Hospitali hiyo Roberty Onesmo zilisema muuaji huyo, Charles Range Kichune (38) alifariki dunia akiwa amelazwa katika wodi namba 8 Hospitalini hapo.
Onesmo alisema kuwa marehemu huyo ambaye mwili wake umehifadhi katika chumba cha kuhifadhia maiti, alifariki muda mfupi majira ya saa 10.00 usiku wa kuamkia juzi, baada ya kufikishwa na askari Polisi.
Mhalifu huyo ambaye ni mkaazi wa kitongoji cha Ronga kijiji cha Kenyamanyori kata ya Turwa wilaya ya Tarime, alikamatwa na askari Polisi mkoani Tanga alikotorokea baada ya kufanya mauaji ya watu tisa na kuwajeruhi wengine na kisha kuwapora vitu mabli mbali.
Jeshi la Polisi Tarime na Rorya na askari wa mkoa wa Tanga kwa ushirikiano walifanikiwa kumkamata siku ya Februali 6, mwaka huu jioni baada ya kukimbia wilayani hapa, alipojificha kwa muda kwa rafiki yake, mhalifu Marwa Keryoba wa mtaa wa Nyabisare manispaa ya Musoma.
Katika upekuzi nyumbani kwa rafiki yake ambaye aliuawa na askari polisi Februali 7 mwaka huu asubuhi katika mtaa huo, baada ya kukaidi amri na kuwarushia risasi, kulikutwa silaha ya aina ya SMG iliyokatwa kitako na mtutu ambayo Charles Range Kichune maarufu ‘’KENONKE’ alikiri kuitumia katika matukio ya mauaji na unyan’ganyi kwa wananchi 9.
Muuaji huyo alikiri kuifunga tochi silaha hiyo iliyotumika kumulika wakati wa kuendesha matukio hayo ambapo miongoni mwa watu waliouawa ni pamoja na mstaafu wa Jeshi la wananchi (Jwtz) na komando ambaye ni mtoto wa marehemu Meja Jenerali Mwita Marwa (Wabachira).
Kamanda wa Polisi Tarime na Rorya Justus Kamugisha alithibitisha kukamatwa kwa muuaji huyo mkoani Tanga, na silaha hiyo ya kivita pamoja na simu na vitu mbali mbali alivyovipora kwa watu waliouawa na kujeruhiwa katika vijiji vya Mogabiri, mjini Tarime, Nkende ,Rebu na Nyamwaga.
Aidha kamanda Kamugisha alithibitisha kufariki dunia muuaji huyo katika Hospitali hiyo baada ya kupelekwa kupatiwa matibabu na kwamba Jeshi la Polisi Tarime na Rorya linaendelea kuwasaka wahalifu wengine.

0 comments:

Post a Comment