Friday, February 7, 2014


Na Gladness Mallya
WIMBI la wasanii kuingia kwenye siasa limeendelea kushika kasi ambapo awamu hii msanii wa maigizo na filamu Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ ametangaza kugombea ubunge kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015.
Msanii wa maigizo na filamu Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’.
‘Akistorisha’ na paparazi wetu, Dude alisema kutokana na sanaa kutotoa masilahi ipasavyo, ameamua kuingia kwenye ulingo wa siasa ambapo anatarajia ‘kunyakua’ Jimbo la Tabora Mjini ambalo kwa sasa linaongozwa na Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage.
“Natarajia kugombea ubunge nyumbani kwetu Tabora mjini, niko tayari kuchuana na Rage na kwa sasa  nipo katika maandalizi ikiwemo kuwa karibu na wananchi kwani  wananikubali sana, hivyo natarajia ushindi tu,” alisema Dude.

0 comments:

Post a Comment